WANAFUNZI WA IITMZ KUNUFAIKA NA MAFUNZO YA VITENDO KUPITIA USHIRIKIANO NA VIGOR
Na Mwatima Issa – IITMZ
Taasisi ya
Teknlojia ya India Madras Kampasi ya Zanzibar (IITMZ) inaendeleza kutimiza
lengo lake la kuhitimisha wataalamu wanaokubalika katika soko la ajira la
Kimataifa, Hayo yameibuka katika kikao cha mazungumzo ya pamoja kilichofanyika
baina ya uongozi wa IITMZ na kampuni ya Vigor Group of Campanies kilichofanyika
katika ofisi za Vigor Migombani mapema wiki hii.
Akizunguma katika
kikao hicho Mkuu wa Taaluma wa Taasisi ya IITMZ Prof. Suresh Akhihebbal amesema
itakuwa ni jambo jema wanafunzi wa IITMZ kutumia taaluma yao ya Akili Unde na
Uhandisi wa viwanda kwa kuwa sehemu wa uzalishaji katika miradi mbalimbali inayosimamiwa na kuendeshwa na Kampuni ya VIGOR hasa ikizingatiwa kuwa wamefikia
hatua ya kutoa mchango wao wa moja kwa moja katika soko la ajira.
Ameendeza kwa
kusema kuwa, kwa sasa wanafunzi ya IITMZ wameanza kutumika katika taasisi
mbalimbali kusaidia katika uendeshaji na uzalishaji wa mifumo ikiwa ndio sehemu
kubwa ya taaluma yao kadhalika kuibua miradi kadhaa yenye tija katika katika
taasisi hizo. Aidha amethibithisha kua
hayo hujitokeza katika mafunzo ya vitendo wanayoshiriki kila wakati wa
mapumziko yao ya muhula wa masomo ya darasani.
Prof.
Suresh ameithibitishia VIGOR kuwa mbali na vijana hao kubakiwa na muda mfupi tu
hadi kuhitimu mafunzo yao ya Shahada ya kwanza ya miaka minne ifikapo mwezi
Julai mwaka 2027, IITMZ itahakikisha wanatumia elimu waliyoipata kuleta mchango
chanya katika maendeleo ya jamii, sekta ya teknolojia na uchumi wa nchi kwa
ujumla.
Amesema
taasisi hiyo itaendelea kuwajengea uwezo wa kitaaluma, ubunifu na uongozi ili
wawe wataalamu wenye ushindani wa kimataifa na wenye uwezo wa kutoa suluhisho
kwa changamoto mbalimbali za kisasa.
Naye
Mtendaji Mkuu, wa Mradi wa ONIRIA kupitia Kampuni ya VIGOR Yulia Baystrukova ameonesha furaha yake
ya wasaa wa mazungumzo hayo na IITMZ na kusema fursa ya uwasilishaji wa shughuli za uzalishaji viwandani pamoja na
dira ya uwekezaji wa mradi wa ONIRIA uliofanyika katika kikao hicho ni ya matumaini.
Amesema
‘Tumefurahishwa sana na majadiliano yaliyofanyika, ambayo yameonesha uwepo wa
nafasi kubwa ya kujenga ushirikiano wa muda mrefu na wenye manufaa kati ya IITM Zanzibar na VIGOR
Group katika maeneo mbalimbali ya maendeleo, ubunifu na teknolojia”.
Aidha Baystrukova
amethibisha, kujenga na kuendeleza ushirikiano huu unaolenga kutoa fursa muhimu
ya mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi kupitia uelewa wa moja kwa moja wa
shughuli halisi za uzalishaji viwandani, mifumo ya uzalishaji, usafirishaji wa
bidhaa, udhibiti wa ubora pamoja na michakato mbalimbali ya viwandani, hususan
kwa programu za Uhandisi wa Kemikali na taaluma nyingine zinazohusiana.
Wakati huo huo, amethibitisha ushiriki wa tukio
la IITMZ la linalotarajiwa kufanyika fanyika tarehe 9 Juni pamoja na
wawakilishi kutoka viwanda na taasisi mbalimbali za uzalishaji. Tukio hilo
litakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya uzalishaji na viwanda linalenga kuzindua programu mpya ya Shahada ya Sayansi
katika masuala ya Uhandisi wa Michakato ya Kemikali (BS in Chemical Process
Engineering) katika Kampasi ya IITM Madras
Zanzibar.
Lengo la tukio hili ni kuwasilisha vipengele
muhimu vya programu hiyo pamoja na kupokea maoni na mapendekezo kuhusu maeneo
mbalimbali yanayohusiana nayo. Aidha, tukio hilo litapambwa na mada mbalimbali
zitakazowasilishwa na viongozi kutoka sekta za viwanda na taaluma za kitaaluma.
Kikao hicho cha mashirikiano ya kiutendaji
kimebainisha vipengele vya kimashirikiano katika kuendeleza utendaji kazi wa
pamoja wa IITMZ na Kampuni ya VIGOR. Maeneo hayo ni uendeshaji wa ziara za
viwandani kwa ajili ya kuwajengea wanafunzi uzoefu wa moja kwa moja katika
mazingira halisi ya uzalishaji, pamoja na programu za udhamini wa elimu na
mafunzo maalum kwa viongozi na wataalamu.
Aidha, ushirikiano huo unatarajiwa kuimarisha
shughuli za michezo na maendeleo ya kijamii, huku pia ukitoa nafasi za mafunzo
kwa vitendo (internships) na kukuza ubunifu kupitia miradi ya pamoja kati ya
sekta ya elimu na viwanda.
Watendaji wa Taasisi ya Teknlojia ya India Madras Kampasi ya Zanzibar
(IITMZ) wakifatilia uwasilishaji wa Taarifa ya za uendeshaji wa Miradi
mbalimbali inayosimamiwa na kuendeshwa na Kampuni ya VIGOR Group of Companies
kufuatia ziara fupi iliyofanywa na viongozi hao wa IITMZ katika ofisi za
kampuni hiyo huko Migombani mapema wiki hii.
Post a Comment