TUNATAKA WANDISHI WA HABARI MJILINDE -UTPC


NA MARYAM NASSOR

WANDISHI  wa Habari wametakiwa kuzingatia usalama wao kwanza wakati wakitimiza majukumu yao  kuelekea kipindi cha uchaguzi   mkuu wa Oktoba mwaka huu 2025.

Akitoa mafunzo  kwa wandishi wa Habari 15  kutoka klabu za wandishi wa Habari huko mjini Morogoro Mkufunzi katika mafunzo hayo Neville  Meena .

Amesema ,  mwandishi wa Habari  usalama wake ni muhimu , tishio lolote   likimpata  mwandishi litasababisha kazi anayotaka kuifanya asiifanye  ipasavyo.

 “ Kwa hiyo tunawataka wandishi wa Habari  kuwa salama  kwa namna moja au nyengine  na usalama wenu   ndio  utasababisha ujumbe munaotaka kuufikisha  kwa jamii  kufika  kwa urahisi.” amesema Meena.

Amesema kuwa,   wanahitaji mwandishi wa Habari asipate  shida yoyote kama kupigwa , kunyang’anywa vifaa , kuumizwa na  hata tatizo la kutekwa na kuumia .

“ Kuna mwandishi mwenzetu   Azori Mziwanda   alipotea siku nyingi zilizopita  na hatujui  alipo , hivyo tunataka kesi kama hizo zisijirudie tena ” amesema Meena.

 Aidha amesema kuwa, usalama wa mwandishi wa Habari unaanza na yeye mwenyewe , kujitambua yeye ni nani anafanya kazi nan ani na mambo mengine mengi ili achukuwe tahadhari mapema na asijikute ameingia katika matatizo yatakayo mfanya asifanye kazi au kutekeleza wajibu wake.

Nae,  Lulu George Mtaalamu wa Maswala ya Saikolojia na mkufunzi katika mafunzo hayo ,amesema  kuwa ni kweli wandishi wa Habari wanakutana na matatizo mbali mbali yanayohusu maswala ya kisaikolojia na wahanga wakuu kutokana na kazi wanazozifanya.

Amesema kuwa, wandishi ndio wanaoripoti  majanga mbali mbali yakiwemo ajali kwa afya ya akili inakuwa ni tatizo lakini kutokana na hali zao wanakosa msaada wa kitaalamu kwa sababu unahitaji gharama na hakuna mtu wa kuwasemea wala kuwapigania.

“ Katika mafunzo haya tumewafundisha ustawi wa afya zao ikiwemo kimwili na akili ili waweze kujilinda na kutekeleza majukumu yao” amesema Lulu.


Victor Maleko  Afisa Mafunzo  kutoka UTPC  amesema  mafunzo hayo yamelenga wandishi wa Habari ambao wataenda kutoa mafunzo kwa  wandishi wengine    kuhusu usalama wa kimtandao, kisaikolojia na usalama wa kimwili .

Amesema kuwa, kitu kilichomfurahisha katika mafunzo hayo  ni kuona  kuwa Ushahidi  wa matukio ambayo yalishawahi kuwapata wandishi wengine wa Habari na kuweza kuyatatua .  

“ Nimefurahi kwa kuweza kupata timu nzuri ya wandishi wa Habari hawa waliyopatiwa mafunzo  naamini wakienda huko katika mikoa waliyotoka wataweza kuifikisha elimu na ujuzi waliyoupata hapa”

Aidha ameendelea kuwasihi wandishi wa Habari kuendelea kubaki  katika  mazingira  salama  na rafiki wakati wakitimiza wajibu wao, na kuwaasa  kuwa usalama wa  mwandishi wa Habari unaanza na  yeye  mwenyewe.



 
Nao,baadhi ya Wandishi wa Habari waliyopata  mafunzo hayo wameahidi kuifikisha elimu hiyo kwa wandishi wenzao katika klabu zao na wandishi wengine wenye uhitaji.

Aidha wameishukuru UTPC  kwa kuwachaguwa wao kuwa sehemu ya wakunzi ( TOT) ambao wataenda kuwafundisha  wenzao.  

Mafunzo hayo ya siku tatu yamewashirikisha wandishi wa Habari 15  kutoka katika klabu za wandishi wa Habari mbali mbali Tanzania, yameandaliwa na Umoja wa  Klabu za Wandishi wa Habari Tanzania  (UTPC).

No comments

Powered by Blogger.